Sunday, August 10, 2008

Taarifa ya Maabara: Ugonjwa Uliomuua Amina Chifupa.

Ugonjwa uliomuua Amina! 2007/07/13 
 
      Ugonjwa huu mpya ambao aliugua Bi. Chifupa na uliosababisha mauti
yake kwa jina la kitaalamu hujulikana kama
 
  "Uumbuajiasis Viongozitanzanialitis Hadharanum."
 
Ugonjwa huu unatokana na kufuatilia mambo ya serikali na
viongozi kwa karibu kiasi cha kutaka kuweka ubovu wao hadharani.
 
Dalili kubwa za ugonjwa huu ni hizi:
 
a. Kupenda nchi zaidi kuliko chama
 
b. Kuwa tayari kutetea mali ya Taifa na kuilinda mali hiyo
 
c. Kutoogopa yatakayokukuta
 
d. Kuanza kuweka hadharani ubovu na siri za viongozi hasa kwa jamaa
   yako karibu
 
e. Kutosikiliza ushauri wa kutakiwa kukaa kimya na wakubwa wako
 
f. Kuwa kimbelembele kuzungumza na kukemea maovu kila upatapo nafasi
 
g. Kuwa mtetezi wa Katiba na mkosoaji wa jamii
 
h. Kutolegeza msimamo hadi kifo.
 
Maambukizi:
Ugonjwa huu unaambukiza watu wachache kwani watu wengi wameshapatiwa
kinga yake. Kwa wale wanaombukizwa wanafanya hivyo zaidi kwa kusoma habari za ufisadi, rushwa, na ubadhirifu katika serikali yao . Kwa kupitia
mitandao, vitabu, na vyombo vya habari ,  virusi vya ugonjwa huu vinajipenyeza katika akili za watu na kusababisha kusisimka kwa ubongo.
Wale waliombukizwa ugonjwa huu hujikuta wakitafuta habari za kila namna
na kushiriki mijadala yenye kutafakari mustakabali wa Taifa lao.
 
Kinga:
Ugonjwa huu kinga yake kubwa hujulikana kwa kitaalamu kama Mlungura.
Kinga hii hutolewa kwa wale wote wenye kuanza kuonesha dalili za kukumbwa na ugonjwa huu.
 
Kinga hii huwekwa kwenye mabenki na maofisi
mbalimbali ili kuzuia viongozi wakubwa wasipatwe na virusi vya
ugonjwa huu. Kinga hii pia hufanya kazi kwa wale walioanza kuonesha dalili kama kina  Zitto, Marmo, Mzindakaya, Slaa, Rev. Mtikila  n.k
 
Pindi mtu akishapatiwa kinga hii
HAWEZI kuipinga serikali!
 
Tiba:
Hadi hivi sasa ugonjwa huu hauna tiba ya uhakika kwani wale ambao
wameshaugua kwa muda mrefu hawako tayari kutibiwa kwani wanaona
wanaishi vizuri tu na ugonjwa huu.
 
Karantini:
Pindi baadhi ya wakubwa wakiona kuna mtu ambaye amefikia hatua ya
juu kabisa ya ugonjwa huu basi kwa mbinu wanazozijua wenyewe
wanamkarantini, na wakati mwingine anakuwa katika hali hiyo ya
kutengwa hadi kifo ili asiendelee kuwaambukiza watu wengine.
 
 Jihadhari:
Kwa vile ugonjwa huu ni wa hatari, watu wabadhirifu, wezi wa mali ya
umma, walaghai, na mafisadi hawawezi kuustahimili.
 
Ugonjwa huu ni kinyume kabisa na watu hawa hivyo kama hutaki kuambuzizwa hakikisha unaendelea
kujikita katika katika vitendo viovu vya kuharibu mali za umma na
kuivunja vunja nchi huku ukishiriki katika kumegeana hazina ya
Taifa.
 
Kwa vile ugonjwa huu unaendelea kuambukiza taratibu, kuna
kila dalili hapo ulipo UNAISHI NA MWATHIRIKA!
  Zinduka,  Kapime ujue afya yako ugonjwa huu upo


"...the path of the righteous man
is beset on the tyranny and inequities
of evil men..."

No comments:

Mambo ya kawaida jamani...

Kama unaona kuwa kuna kitu kinakufurahisha humu kwenye blog yangu basi hakuna noma kama ukiniangushia sifa mwanangu mwenyewe.....
Washkaji Mungu akipenda tutaonana basi.........ila kumbuka kuwa Mungu ni mmoja na siku zote anafanya maajabu kwahiyo si mbaya kama tukimshuru kwa kila nia.....
Mungu awabariki watu wote wa Dunia hii.Amen!

9 Things I Hate About Everyone

1. People who point at their wrist while asking for the time.... I know where my watch is pal, where the hell is yours? Do I point at my crotch when I ask where the toilet is?



2
 People who are willing to get off their ass to search the entire room for the T.V.. remote because they refuse to walk to the T.V. and change the channel manually. 

3
 When people say 'Oh you just want to have your cake and eat it too'. Damn right! What good is cake if you can't eat it? 

4
 When people say 'it's always the last place you look'. Of course it is. Why the hell would you keep looking after you've found it? Do people do this? Who and where are they?   cause I amGonna Kick their asses! 

5
 When people say while watching a film 'did you see that?'. No Loser, I paid $12 to come to the cinema and stare at the damn floor. 

6
 People who ask 'Can I ask you a question?'.... Didn't really give me a choice there, did ya sunshine? 


7.
 When something is 'new and improved!'. Which is it? If it's new, then there has never been anything before it. If it's an improvement, then there must have been something before it, couldn't be new.

8
 When people say 'life is short'. What the hell?? Life is the longest damn thing anyone ever does!! What can you do that's longer?




9
 When you are waiting for the bus and someone asks 'Has the bus come yet?'. If the bus came would I be standing here, dumbass? 

 

If you are having a bad day, remember it could be worse...

If you are having a bad day,  remember it could be worse...