Saturday, January 16, 2010

Is happening tonight!

Ndugu yetu Eugine Makupa a.k.a King Kupa anawataarifu ndugu, jamaa na marafiki wake kwamba atakuwa na maombi mafupi nyumbani kwake leo saa mbili usiku. Angependa sana kama wewe na mimi tungeweza kujumuika naye ili kuweza kumwombea mama yake mzazi Mrs. Bernadine Makupa aliyefariki dunia Jumatatu ya tarehe 8 huko Kilimanjaro, Tanzania.

Kama ilivyo kawaida yetu, basi kama unachochote kile si vibaya kukileta siku hii ya leo. Kwa habari kamili kuhusu maombi haya, unaweza kuzipata kwa kuwasiliana na mdau Solomon a.k.a DJ Smilez kwa namba ya simu ya mkononi...316 347 9773. Tunatanguliza shukrani zetu zote za dhati kwa wewe uliyesoma message hii. Please let some else know about this. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi...Amen.

Republic of Zimbabwe (GDP – per capita: $500)

“The expression on these guys faces says a million things, weak from hunger and too poor to own shoes or have a shirt to wear. This is all because of the tyrant they call a president.

A beautiful country ruined because of one mans greed. ” Mr Sean

Republic of Zimbabwe is located between the Limpopo and Zambezi rivers in the south of Africa. Its economy suffers a slowdown due to supply shortage, soaring inflation and foreign exchange shortage. Zimbabwe’s involvement in the Democratic Republic of the Congo left its economy fragile. The worst consequence of the knelt-down economy is unemployment that is as high as 80%.

“March, 5, 2008. The Zimbabwean currency tumbled to a record 25 million dollars for a single US dollar”

Osama Bin Laden Alivyo Sasa!

Pinda atangaza mali zake...

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda ametangaza mali zake alizonazo anazozimiliki mbele ya vyombo vya habari ofisini kwake jana.
Pinda alitangaza mali hizo zikiwemo na shilingi milioni 25 kwenye akaunti yake, nyumba tatu za kawaida moja ikiwa jijini Dar es Salaam, Mpanda na Dodoma na gari moja alilolinunua kwa mkopo.

Waziri Pinda aliamua kufanya hivyo ili kuweka bayana mali zake na kuonyesha mfano kwa viongozi wote nchini kufata kwa kuwa viongozi walitakiwa kuweka bayana mali zao ili kutekeleza sheria ya maadili ya uongozi.

"Hizo ndizo mali zangu nilizo nazo ndugu" alisema mbunge huyo wa Mpanda wakati akitangaza mali zake

Waziri mkuu aliyetambulika kwa jina la mtoto wa mkulima alitaja mali zake hizo na kusema haelewi yeye kwake utajiri ni nini na kusema mali hizo kwake anajiona ni tayari zimeshamtosheleza na wakati akianza kutaja mali zake hizo wka kujielezea mbele za wahariri alianza kwa kusema

"Nina nyumba Dodoma kutokana na utaratibu wa mikopo ya nyumba za serikali; nina nyumba Mpanda ambayo imepatikana kwa mpango wa kawaida tu, imetokana na visenti kidogo nikanunua pale ambapo bahati nzuri gharama za ujenzi hazikuwa kubwa sana, nikakikarabati kipo pale kipo Makanyagio pale."

"Haya! Ukitoka pale unataka niseme nini tena. Dar es Salaam sina nyumba ya kusema ya maana sana ukienda shambani Pugu kule kipo kinyumba kidogo hivyo inahitajika kazi ya ziada kuweza kufanya paonekane pa maana.

"Kijijini kwa baba yangu pale Kibaoni sina nyumba; pale mlipoona nimekaa na bibi tunapiga porojo, kile kijumba mimi na wadogo zangu tulimsaidia babu kwa ajili ya kumjengea babu yetu na pale ndipo nilipokuwa nafikia siku zote wakati wa likizo."

Pinda, ambaye amekuwa mbunge tangu mwaka 2000, alisema miaka yote alikuwa akifikia kwenye nyumba hiyo ambayo yeye ana chumba chake kimoja hali kadhalika babu yake.

Alisema baada ya kuteuliwa kuwa waziri mkuu, alijikuta kwenye wakati mgumu sana kwa kuwa alitaka kuendelea kufikia kwenye nyumba hiyo, lakini watu wa usalama walimkataza.

"Baada ya hii maneno inayoitwa uwaziri mkuu, nilipoteuliwa nikataka nifikie pale katika ile nyumba, lakini nikaambiwa hapana; haiwezekani; hapafai; huwezi kufikia pale,"alisema.
Alisema hilo ndilo lilikuwa tatizo lake la kwanza kwa hiyo anajaribu kujenga tena kitu ambacho na yeye atapata mahala pa kufikia pamoja na wasaidizi wake kwenye eneo hilo.

"Nimegundua tatizo ni hawa wakubwa. Pale kijijini kwetu hakuna nyumba za wageni hatuna chochote mi nilidhani nikienda kule nikiachwa kwa babu na bibi, wao wataenda huko umbali wa kilomita wakatafute pa kupumzika, lakini wakasema no! no! no! haiwezekani, nikawaelewa," alisema.

Alisema ukiondoa nyumba hiyo, vitu vya maana zaidi hana labda gari la mkopo na ni gari la mbunge.
Pinda aliendelea kuwaambia wahariri kuwa

"Hivi ukifika hivi unahitaji nini cha zaidi tena? Kwa hiyo kipato kidogo unachokipata unaweza kukitumia kwa ajili ya huduma za watoto wako kusoma na kadhalika kwa sababu ni vitu viko nje ya taratibu za serikali. Kwa hiyo huwa najiona tu kwamba na mimi nina bahati tu kwamba Mungu alinifikisha hapa nilipofika na kunifikisha katika nafasi hii imenipa ahueni," alisema.

Alisema kama masuala hayo muhimu yanatimia, wajibu wake ni kujaribu kulipa fadhila kwa Watanzania kwa kufanya kila atakaloweza kuwatumikia vizuri zaidi.

"Kwa hiyo mimi nina hakika zaidi kuwa kwa nafasi kama niliyo nayo, naweza kuishi bila tamaa ya mambo mengine zaidi... mimi hata hisa sina, sijanunua hisa mahali popote, lakini huko tunakokwenda naweza nikatamani nikatafuta hata hisa hivi, kwa ajili labda ya sababu fulani fulani," alisema.



I WANNA HEAR FROM YOU!

Juu ya fish tank kuna lotion, kwa kweli bado sijajua inafanya nini pale. Naomba sana wafurukutwa mnisaidie kama mna any comments. Na kwa data ambazo zipo mtaani ni kwamba ile lotion inapungua every other day. Please my sisters and brothers nisaidieni hapo bwana.... Kunani pale?!

SIRI IMEFICHUKA!

Sasa tumegundua ni nini hasa kinamfanya mdau huyu wa kushoto hapa katika picha kunawiri na kujinenepea kama akina mimi, Ni chupa za Kijani. Yaani mdau ni mzima kwenye hiyo sekta. Kushoto ni tapeli Ngassa D akiwa anajitahidi kutosinzia kabisa kwani ilikuwa ni usiku wa kiza kinene. Be careful ukimwona mdau huyu wa kulia kwani huwaga na plans za faster sana na ukizubaa utajikuta huna wa kumlaumu.

Look at this man!

Huyu kijana wa kulia kabisa ni Salehe a.k.a Kanye West yaani ametulia kabisa kusubira photo. Watu kama hawa ni wazushi tu kwani anaonekana kama vile hana mpango na issues ambazo viongozi wanaziongelea pale. Ila kwa mujibu wa watu walio karibu na Salehe ni kwamba kwa sasa anamalizia single yake mpya ya "I'm from Kisarawe" ambayo atamshirikia Ali Kiba katika kiitikio... Kila la Heri mheshimiwa.

Wasiovuma lakini wamo...

Mdau anaonekana anafuraha sana yaani. Kweli mwaka 2010 si mbaya kwake kwani unaona meno ya mbwa yote nje na kujitanua kwa kwenda mbele...Hii ni safi sana. Kwa data ambazo tunazo kwenye ofisi zetu ni kwamba mdau huyu kwa sasa ana plans za kwenda nyumbani Bongo na kugombea kiti cha Ubunge wa Kilwa. Tutapost more updates kwa jinsi tunavyozipata.

Mambo ya kawaida jamani...

Kama unaona kuwa kuna kitu kinakufurahisha humu kwenye blog yangu basi hakuna noma kama ukiniangushia sifa mwanangu mwenyewe.....
Washkaji Mungu akipenda tutaonana basi.........ila kumbuka kuwa Mungu ni mmoja na siku zote anafanya maajabu kwahiyo si mbaya kama tukimshuru kwa kila nia.....
Mungu awabariki watu wote wa Dunia hii.Amen!

9 Things I Hate About Everyone

1. People who point at their wrist while asking for the time.... I know where my watch is pal, where the hell is yours? Do I point at my crotch when I ask where the toilet is?



2
 People who are willing to get off their ass to search the entire room for the T.V.. remote because they refuse to walk to the T.V. and change the channel manually. 

3
 When people say 'Oh you just want to have your cake and eat it too'. Damn right! What good is cake if you can't eat it? 

4
 When people say 'it's always the last place you look'. Of course it is. Why the hell would you keep looking after you've found it? Do people do this? Who and where are they?   cause I amGonna Kick their asses! 

5
 When people say while watching a film 'did you see that?'. No Loser, I paid $12 to come to the cinema and stare at the damn floor. 

6
 People who ask 'Can I ask you a question?'.... Didn't really give me a choice there, did ya sunshine? 


7.
 When something is 'new and improved!'. Which is it? If it's new, then there has never been anything before it. If it's an improvement, then there must have been something before it, couldn't be new.

8
 When people say 'life is short'. What the hell?? Life is the longest damn thing anyone ever does!! What can you do that's longer?




9
 When you are waiting for the bus and someone asks 'Has the bus come yet?'. If the bus came would I be standing here, dumbass? 

 

If you are having a bad day, remember it could be worse...

If you are having a bad day,  remember it could be worse...